Yanga: zoezi la utolewaji Fomu

Zoezi la utolewaji wa fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi wa Yanga linatarajiwa kufungwa leo Jumatano, Novemba 14 2018 ambapo mpaka sasa watu 12 wamejitokeza kuchukua fomu.

Licha ya uongozi wa Yanga kusisitiza kuendelea kumtambua Mwenyekiti Yusufu Manji, Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limesema haliyatambui maamuzi hayo na limeendelea na mchakato wa uchaguzi utakaohusisha nafasi hiyo ya Mwenyekiti.

Jana TFF imewafungia kutojihusiaha na soka nchini kwa miaka mitatu viongozi wa Matawi Yanga, Mwenyekiti Bakili Makele na Katibu Boaz Ikupilika baada ya kuwapata na hatia ya kupinga mchakato wa uchaguzi unaoendelea

Mpaka sasa aliyejitokeza kuwania Uwenyekiti wa Yanga ni Jonas Tiboroha, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga.

Yono Kevela yeye amechukua fomu ya kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti.

Waliochukua fomu kuwania nafasi nne za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Hamad Ally, Benjamin Jackson, Silvestoer Haule, Musa Katabaro, Said Baraka, Pindu Luhoyo, Dominic Francis na Jeko Jihadhari.