Klabu ya Polisi Tanzania inayoshiriki ligi daraja la kwanza imetuma maombi kwa Yanga kuwataka kwa mkopo wachezaji wawili Yusufu Mhilu na Baruani Akilimali imefahamika.
Maneja wa Polisi, Nelson Ngonyani amethibitisha timu yake kuwataka wachezaji hao ambao wamekuwa na wakati mgumu kupata nafasi kwenye kikosi cha Mwinyi Zahera
Yanga ilishaweka wazi kuwa inakusudia kuwatoa kwa mkopo baadhi ya wachezaji wake chipukizi ambao wamekosa nafasi
Mbali na wachezaji hao, wengine ambao wamekuwa hawapati nafasi na wanaweza wakatolewa kwa mkopo ni pamoja na Ramadhani Kabwili, Emmanuel Martin, Pius Buswita na Yohana Mkomola