TFF: Hatumtambui MANJI lazima Uchaguzi Ufanyike

Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF mchana huu limesema kuwa hawatambui kurejea kwa aliyekuwa mwenyekiti wa Yanga Sc Yusuph Manji hivyo uchaguzi utafanyika kama kawaida. .
.
Aidha shirikisho hilo limesisitiza mbele ya waandishi wa habari kuwa zoezi la kuchukua fomu kwaajili ya wagombea wanaowania nafasi zilizowazi ndani ya klabu hiyo linaendelea hivyo kama wanayanga wanamtaka Manji basi achukue fomu na kama wana Yanga wanamtaka basi atapita bila wasiwasi ila cha msingi uchaguzi kufanyika. .
.
Mbali na hilo TFF wamefika mbali zaidi na kusema wamepata taarifa za mkutano wa dharura wa Yanga wanaotarajia kuufanya November 24 na kuhudhuriwa na Yusuph manji, hivyo Manji anatakiwa kuhudhuria kama mwanachama wa Yanga na si kama Mwenyekiti kwani wao wanatambua nafasi ya Mwenyekiti ndani ya Yanga Sc iko wazi.
.
.
Katika hatua nyingine shirikisho hilo limesema litakuwa tayari kushirikiana na kamati ya uchaguzi ya Yanga Sc kusimamia zoezi zima la uchaguzi na si kuwaachia kama wao wanavyotaka kwakuwa walishapata barua kadhaa kutoka TFF kuwataka wafanye uchaguzi lakini hawakufanya, hivyo ni wakati wa TFF kusimamia suala hilo.
#sokaonlineUpdates