Simba 0-0 Nyasa Big Bullets : Full Time

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba wamelazimishwa suluhu ya bila kufungana na mabingwa wa Malawi, Nyasa Big Bullets katika mchezo wa kirafiki uliopigwa uwanja wa Taifa Ijumaa jioni.

Mchezo huo uliokuwa maalum kuziandaa timu hizo kwa ajili ya michezo ya awali ya ligi ya mabingwa inayopigwa mwishoni mwa mwezi huu, ulishuhudia kosakosa za hapa na pale kutoka kila upande huku Simba ikitawala kwa muda mwingi.

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems aliutumia mchezo huo kuwapa nafasi baadhi ya wachezaji ambao hawamo kwenye kikosi cha kwanza baada ya idadi kubwa ya wachezaji wa Simba (12) kuitwa kwenye timu za Taifa.

Simba inatarajiwa kucheza mchezo mwingine wa kirafiki kabla ya kuivaa Mbabane Swallows mwishoni mwa mwezi huu.