Simba kuharakisha USAJILI wa Beki Wa Kulia

Kuumia kwa Shomari Kapombe kumewafanya mabosi wa Kamati ya usajili ya klabu ya Simba kuharakisha usajili wa mbadala wake imefahamika.

Kapombe alipata majeraha makubwa akiwa kwenye kambi ya timu ya Taifa nchini Afrika Kusini na upo uwezekano akawa nje kwa muda mrefu.

Msimu uliopita Nicolas Gyan alitumika kwenye nafasi hiyo kwa nyakati tofauti, hata hivyo ameshindwa kumshawishi kocha Patrick Aussems.

Gyan hajajumuishwa katika kikosi cha Simba kitakachoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa inayoanza mwishoni mwa mwezi huu.

Katika mchezo wa kirafiki kati ya Simba dhidi ya Nyasa Big Bullets uliopigwa Ijumaa iliyopita, Aussems alimtumia Yusufu Mlipili kama beki wa kulia.

Hata hivyo Mlipili alishindwa kuimudu nafasi hiyo.

Wakati Simba ikiendelea na mchakato wa kusajili mlinzi wa kulia, huenda kiraka Erasto Nyoni akarejeshwa kwenye nafasi hiyo.

Nyoni ana uwezo wa kucheza nafasi zote za ulinzi na kiungo.

Simba inahusishwa na beki wa Tanzania Prisons Salum Kimenya ambaye amekiri kuwa katika mazungumzo na uongozi wa Simba