Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kimewasili leo Jumatatu jioni kutoka nchini Lesotho kwenye mchezo wa kuitafuta tiketi ya kucheza Fainali za Africa 2019.
Stars imerejea ikiwa na majonzi baada ya kupoteza mchezo muhimu dhidi ya Lesotho kwa kukubali kichapo cha bao 1-0 na kufifisha matumaini ya kufuzu fainali za AFCON 2019
Mchezo wa mwisho kundi L unatarajiwa kupiga mwezi March 2019 dhidi ya Uganda.
Ushindi katika mchezo huo unaweza kuipa Stars nafasi ya kufuzu iwapo Lesotho itashindwa kupata ushindi dhidi ya Cape Verde ugenini