Yondani, Kakolanya waikosa Safari ya Shinyanga

Yanga itashuka uwanja wa Kamabarage mkoani Shinyanga keshokutwa Alhamisi, Novemba 22 2018 kumenyana na Mwadui Fc kwenye mchezo wa kiporo wa ligi kuu ya Tanzania Bara.

Kikosi cha Yanga kimeondoka Alfajiri ya leo kwa usafiri wa Ndege mpaka Mwanza ambako kimechukua usafiri wa basi kuelekea mkoani Shinyanga.

Nahodha Kelvin Yondani na Mlinda lango Beno Kakolanya sio miongoni mwa wachezaji waliosafiri baada ya kushindwa kuripoti kambini kwa wakati.

Wachezaji hao waliokuwa na timu ya Taifa nchini Lesotho, walipaswa kuwepo kambini kabla ya safari hiyo licha ya kuwasili na kikosi cha Stars jana saa 12 jioni kutoka Afrika Kusini

Gadiel Michael na Feisal Salum inaelezwa wao waliweza kuwahi na wamesafiri.

Yanga pia itawakosa Ramadhani Kabwili, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Paulo Godfrey ‘Boxer’ ambao wako kwenye kikosi cha timu Taifa ya vijana U23 inayoshuka dimbani leo kumenyana na Burundi

Wengine wanaokosekana kutoka na majeraha ni Papi Tshishimbi na Juma Mahadhi ambaye hata hivyo ameanza mazoezi mepesi baada ya kuwa nje kwa miezi mitatu