SIMBA: Mbabane Swallows wametuponza vs Lipuli

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema mawazo ya mchezo wa ligi ya mabingwa kwa wachezaji wake, yamechangia wasifanye vizuri kwenye mchezo wa jana dhidi ya Lipuli fc.

Jana Simba ililazimishwa suluhu ya bila kifungana na Lipuli Fc kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Taifa.

Aussems amesema wachezaji wake walitekwa na mawazo ya mchezo wa ligi ya mabingwa utakaopigwa Jumatano ijayo dhidi ya Mbabane Swallows

“Tulipoteza umakini leo, nadhani wachezaji wangu walitekwa zaidi na fikra za mchezo wa ligi ya mabingwa,” amesema Aussems

Aussems anaamini matokeo ya jana hayataathiri morali ya kikosi chake kuelekea mchezo huo muhimu utakaopigwa Jumatano ijayo kwenye uwanja wa Taifa