Nahodha wa kikosi cha Simba John Bocco amesema wanatambua walikosa ufanisi kwenye mchezo wa ligi jana dhidi ya Lipuli Fc na kulazimishwa suluhu ya bila kufungana.
Bocco ameahidi kurekebisha makosa na amesema anaamini watafanya vizuri kwenye mchezo ujao wa ligi ya mabingwa dhidi ya Mbabane Swallows.
“Haikuwa matarajio yetu kwa matokeo tuliyoyapata, tulijitahidi kutengeneza mashambulizi lakini haikuwa bahati yetu. Tunaangalia kipi tulichokosea, tunaenda kujirekebisha ili tufanye vizuri kwa mchezo unaokuja,” amesema
Bocco amekuwa sehemu kubwa ya mjadala miongoni mwa mashabiki wa Simba tangu jana baada ya kukosa nafasi nyingi za wazi kwenye mchezo dhidi ya Lipuli Fc
Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuendelea na mazoezi kesho kujiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa utakaopigwa kwenye uwanja wa Taifa Jumatano, Novemba 28 2018.