Mabingwa wa kihistoria wa Tanzania, Yanga leo wameendeleza rekodi ya ushindi ugenini kwa asilimia 100 baada ya kuichapa Kagera Sugar mabao 2-1 kwenye mchezo Mabingwa wa kihistoria wa Tanzania, Yanga leo wameendeleza rekodi ya ushindi ugenini kwa asilimia 100 baada ya kuichapa Kagera Sugar mabao 2-1 kwenye mchezo uliopigwa dimba la Kaitaba.
Haritier Makambo ambaye amerejesha makali yake ya kupachika mabao, aliitanguliza Yanga kwenye dakika ya 21 kwa bao safi la kichwa baada ya kuunganisha krosi ya Haji Mwinyi.
Kagera Sugar walisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 32 kupitia mkwaju wa penati uliopigwa na Ramadhani Kapera baada ya mshambuliaji huyo kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari
Katika kipindi cha pili ni Yanga iliyorejea ikiwa na kasi ya kusaka bao la ushindi.
Yanga iliongeza kasi zaidi baada ya mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mwinyi Zahera aliyewatoa Makamnbo aliyepata majeraha na nafasi yake kuchukuliwa na Ibrahim Ajib, Maka aliyetoka kumpisha Raphael Daudi na Haji Mwinyi aliyempisha Deus Kaseke.
Alikuwa ni Lothi aliyeihakikishia Yanga alama tatu muhimu kwenye dakika ya 74 alipounganisha kwa kichwa mpira aliotengenezewa na Deus Kaseke kutoka krosi ya Paulo Godfrey ‘Boxer’ aliyekuwa na mchezo mzuri sana.
Mlinda lango Ramadhani Kabwili leo ameonyesha ukomavu na kudhihirisha kuwa yeye ni chaguo sahihi la kulinda lango mbele na Klaus Kindoki baada ya kuokoa mashambuliz ya hatari wakati mchezo huo ukielekea ukingoni
Matokeo hayo yameikita Yanga kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa imefikisha alama 32, alama tano mbele ya Simba mabayo iko nafasi ya tatu ikiwa na alama 27 huku timu zote zikiwa zimeshuka dimbani mara 12.
Yanga pia iko nyuma ya Azam Fc kwa alama moja tu huku pia ikiwa na mchezo mmoja mkononi.
Ushindi kwenye mchezo ujao dhidi ya JKT Tanzania utakaopigwa kwenye uwanja wa Taifa utaipeleka Yanga kileleni.uliopigwa dimba la Kaitaba.
Haritier Makambo ambaye amerejesha makali yake ya kupachika mabao, aliitanguliza Yanga kwenye dakika ya 21 kwa bao safi la kichwa baada ya kuunganisha krosi ya Haji Mwinyi.

Kagera Sugar walisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 32 kupitia mkwaju wa penati uliopigwa na Ramadhani Kapera baada ya mshambuliaji huyo kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari
Katika kipindi cha pili ni Yanga iliyorejea ikiwa na kasi ya kusaka bao la ushindi.
Yanga iliongeza kasi zaidi baada ya mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mwinyi Zahera aliyewatoa Makamnbo aliyepata majeraha na nafasi yake kuchukuliwa na Ibrahim Ajib, Maka aliyetoka kumpisha Raphael Daudi na Haji Mwinyi aliyempisha Deus Kaseke.
Alikuwa ni Lothi aliyeihakikishia Yanga alama tatu muhimu kwenye dakika ya 74 alipounganisha kwa kichwa mpira aliotengenezewa na Deus Kaseke kutoka krosi ya Paulo Godfrey ‘Boxer’ aliyekuwa na mchezo mzuri sana.
Mlinda lango Ramadhani Kabwili leo ameonyesha ukomavu na kudhihirisha kuwa yeye ni chaguo sahihi la kulinda lango mbele na Klaus Kindoki baada ya kuokoa mashambuliz ya hatari wakati mchezo huo ukielekea ukingoni
Matokeo hayo yameikita Yanga kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa imefikisha alama 32, alama tano mbele ya Simba mabayo iko nafasi ya tatu ikiwa na alama 27 huku timu zote zikiwa zimeshuka dimbani mara 12.
Yanga pia iko nyuma ya Azam Fc kwa alama moja tu huku pia ikiwa na mchezo mmoja mkononi.
Ushindi kwenye mchezo ujao dhidi ya JKT Tanzania utakaopigwa kwenye uwanja wa Taifa utaipeleka Yanga kileleni.
