Licha ya kuchelewa kujiunga na kambi ya Simba kutokana na kukabiliwa na majukumu ya timu ya Taifa, mshambuliaji hatari Emmanuel Okwi jana aliwasili nchini sambamba na beki Juuko Murshidi.
Baada ya kuwasili, moja kwa moja wachezaji hao walielekea kambini kujiunga na wachezaji wengine tayari kwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Mbabane Swallows kesho.
Okwi alishiriki mazoezi ya jana jioni ya kikosi cha Simba na uwepo wake uliongeza ‘mzuka’ kwa mashabiki waliojawa na furaha baada ya kumuona.
Kurejea kwake pia kumeimarisha utimamu wa safu ya ushambuliaji ya Simba ambayo sasa ina uhakika wa kuwavaa Mbabane Swallows ikiwa na majembe yake yote matatu Okwi, Kagere na Bocco.
Kocha Patrick Aussems amesema atamtumia Okwi kwenye mchezo wa kesho kwani katika mazoezi ya jana ameonyesha kuwa yuko ‘fit’