Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba kimeondoka leo Jumapili kuelekea nchini Afrika Kusini ambako kitaunganisha kwenda Eswatini kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa barani Afrika.
Msafara wa mabingwa hao wa kihistoria umejumuisha wachezaji 20 na viongozi nane wa benchi la Ufundi.
Mchezo dhidi ya Mbabane Swallows utapigwa siku ya Jumatano, Disemba 05 huko eSwatini (zamani Swaziland)
Afisa Habari wa Simba Haji Manara amesema wanakwenda kuivaa Mbabane Swallows kwa tahadhari kubwa huku wakifahamu wanahitaji kufuzu kwenda raundi inayofuata.
Jumatano Simba itashuka dimbani ikiwa na faida ya ushindi wa mabao 4-1 iliyopata mapema wiki hii kwenye dimba la Taifa.
