Nahodha wa Yanga Kelvin Yondani amerejea kikosini baada ya kuwa nje kwa zaidi ya wiki tatu akisumbuliwa na majeraha ya enka.
Hivi karibuni Yondani na mlinda lango Beno Kakolanya waliviteka vyombo vya habari za michezo baada ya kudaiwa wamegoma kucheza wakishinikiza walipwe madai yao.
Hata hivyo beki huyo mkongwe alikanusha taarifa hizo na kusisitiza alikuwa akisumbuliwa na majeraha ya enka na uongozi wa Yanga ulikuwa na taarifa zake
Naye kiungo Mcongomani Papi Tshishimbi amerejea kikosini baada ya kupona majeraha.
Tshishimbi, Yondani na winga mpya Reuben Bomba walihudhuria mazoezi ya jana ya kikosi cha Yanga yanayofanyika Chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es salaam.