Mlinda lango wa Yanga Ramadhani Kabwili jana aliruhusiwa kutoka Hospitalini baada ya kufanyiwa vipimo vya jeraha la nyonga alilopata kwenye mchezo dhidi ya African Lyon.
Kabwili alikimbizwa hospitalini baada ya kupata majeraha hayo katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0
“Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu,pili naishukuru klabu yangu kwa kunijali na kuhakikisha napata huduma sahihi,” alisema Kabwili baada ya kuruhusiwa
“Pia awashukuru mashabiki wetu walioungana na mimi hospitalini, mpaka sasa naendelea vizuri.
“Nawapongeza wachezaji wenzangu kwa ushindi wa leo sasa tunaangalia mchezo unaofuata, najisikia vema, Ahsanteni sana”