FT : Azam Fc 1-3 Simba

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wameendeleza wimbi la ushindi kwenye ligi hiyo baada ya leo kuifumua Azam Fc mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa dimba la Taifa

Mapema tu katika dakika ya nne, Meddie Kagere aliifungia Simba bao la kuongoza akimalizia mpira uliokuwa umegonga mwamba ambao ulipigwa na John Bocco

Muda mfupi uliopita, Razak Abarora, mlinda lango wa Azam Fc alinusurika kuokata mpira kimiani baada ya shuti la Clatous Chama kumponyoka mikononi na kuuokota mpira huo katika mstari wakati ukielekea nyavuni

Bocco aliiongezea Simba bao la pili kwenye dakika ya 38 akimalizia kwa kichwa krosi murua ya Zana Coulibaly

Zana ameendelea kun’gara katika kikosi cha Simba, baada ya kuanza kwa kusuasua, sasa uwezo wake unadhihiri

Simba ilikwenda mapumziko ikiongoza kwa mabao 2-0

Katika kipindi cha pili Simba ilipunguza kasi na kuwapa nafasi Azam Fc kutawala mchezo huku vijana wa Aussems wakitumia mashambulizi ya kushitukiza

Kagere aliiongezea Simba bao la tatu kwenye dakika ya 78 akiachia shuti akiwa ndani ya 18

Hilo lilikuwa bao la 11 kwa Kagere sasa akiwa nyuma kwa bao moja dhidi ya vinara wa mabao kwenye ligi Salim Aiyee na Heritier Makambo wenye mabao 12

Bao la kufutia machozi kwa upande wa Azam Fc lilifungwa na Frank Domayo kwenye dakika ya 81

Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama 45, alama tano nyuma ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 50

Hata hivyo Simba ina michezo saba ya viporo

Mchezo unaofuta ni dhidi ya Lipuli Fc utakaopigwa Jumanne ijayo, Februari 26 mkoani Iringa