
Nahodha John Bocco alifunga mabao mawili kwenye mchezo huo huku Adam Salamba naye akifunga bao muhimu ambalo bila shaka litamuongezea kujiamini
Bocco amefikisha mabao sita akiendelea kusogea juu katika kinyan’ganyiro cha kuwania kiatu cha dhahabu

Katika mchezo wa leo kocha Patrick Aussems alifanya mabadiliko ya kikosi chake kwa kuwapumzisha baadhi ya wachezaji huku washambuliaji Emmanuel Okwi na Meddie Kagere wakikosa mchezo huo wakitumikia adhabu ya kadi tatu za njano
Simba imeendelea ikisogea kileleni mwa msimamo wa ligi ikifikisha alama 42 baada ya ushindi huo
Kikosi cha Simba kinatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam kesho kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya Azam Fc utakaopigwa Ijumaa, Februari 22 2019