
Msemaji wa famili Annik Kashasha amesema taratibu za kuuleta mwili zinafanyika nchini Afrika Kusini ambako marehemu alifariki juzi wakati akiendelea na matibabu.
“Mwili wa marehemu utarejeshwa hapa nchini siku ya Ijumaa (Machi 1) na siku ya Jumapili (Machi 3) utasafirishwa kwenda Bukoba kwaajili ya mazishi,” alisema Kashasha
Kifo cha Ruge kimewashtua Watanzania kutokana na mchango wake hasa katika kuwasaidia vijana kutimiza ndoto zao
Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera ni miongoni mwa walioguswa na kifo cha Ruge ambapo amebainisha licha ya kutokumfahamu kabla, amebaini alikuwa ni mtu wa kipekee kwa Watanzania
