
Mchezo huo utapigigwa keshokutwa Jumamosi, March 02 2019 katika uwanja wa CCM Kirumba
Yanga iliondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya leo Alhamisi ikiwa na msafara uliojumuisha wachezaji 20 na viongozi nane wakiwemo wa benchi la ufundi
Baada ya hivi karibuni ‘kuvunja mwiko’ kwa kuchukua alama tatu dhidi ya Mbao Fc katika dimba la CCM Kirumba, Yanga imepania kuchukua alama nyingine tatu mbele ya Alliance Fc
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema anatambua matokeo tofauti na ushindi yatapunguza matumaini ya timu hiyo kutwaa ubingwa hivyo wamejipanga kushinda