FULL TIME: YANGA 1-0 ALLIANCE FC

Vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga wameendelea kujikita kileleni katika msimamo wa ligi baada ya kuichapa Alliance Fc bao 1-0 katika mchezo wa ligi hiyo uliopigwa dimba la CCM Kirumba

Ulikuwa ni mchezo wa ushindani kutoka kwa kila upande ambapo kikosi cha Alliance Fc kimeonekana kuimarika sana tofauti na wakati timu hizo zilipokutana kwenye dimba la Taifa mwaka jana

Bao pekee la Yanga liliwekwa kimiani na mshambuliaji mkongwe Amissi Tambwe kwenye dakika ya 75 ya mchezo

Hilo lilikuwa bao la nane kwa Tambwe msimu huu

Katika mchezo huo Heritier Makambo alikosa mkwaju wa penati mapema tu kwenye dakika ya sita baada ya yeye mwenyewe kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari

Matokeo hayo yameifanya Yanga iendelee kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 64