
Okwi alipata majeraha madogo kwenye mchezo dhidi ya Lipuli Fc. Lakini pia Okwi alicheza mchezo huo huku akiwa amefungwa bandeji chini ya jicho kutokana na jeraha la kuchanika alilopata kwenye mchezo dhidi ya Azam Fc
Baada ya mchezo wa Lipuli Fc, Okwi alirejeshwa jijini Dar es salaam kwa ajili ya matibabu zaidi
Hata hivyo taarifa za uhakika ni kuwa kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amempa mapumziko mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Uganda ili aweze kupona kabisa majeraha yake tayari kwa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya JS Saoura
Baada ya mchezo dhidi ya Stand, Simba itasafiri kwenda Algeria kuikabili JS Saoura kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa hatua ya makundi, raundi ya tano utakaopigwa Jumamosi ijayo, March 09 2019
Simba inahitaji angalau pointi moja tu ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo