
Leo Meddie Kagere anatarajiwa kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Simba kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Stand United utakaopigwa uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga
Kagere mwenye mabao 12, yuko katika kiwango bora cha upachikaji mabao, akifunga mfululizo kwenye michezo mitano iliyopita
“Kazi yangu mimi ni kufunga, hivyo nitaendelea kufanya hivyo kila ninapopata nafasi ili niisaidie timu yangu iweze kupata ushindi,” alisema Kagere baada ya mazoezi ya jana
Kagere ndiye mchezaji hatari zaidi katika ligi kuu ya Tanzania Bara kwa sasa kutokana na kuwa na wastani mzuri wa kufunga kulingana na uwiano wa michezo aliyocheza