RUGE KUPUMZISHWA LEO

Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Vipindi Clouds Media, Ruge Mutahaba unatarajiwa kuzikwa leo katika kijiji cha Kisiru Wilayani Bukoba mkoa wa Kagera

Baada ya kuagwa jijini Dar es salaam, mwili wa Ruge ulisafirishwa jana Jumapili kuelekea Bukoba tayari kwa mazishi hayo

Wananchi wengi walijitokeza uwanja wa Ndege wa Bukoba katika mapokezi ya mwili wa Ruge ambaye enzi za uhai wake alikuwa mtu wa watu

Watu wengi wamesafiri kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania kwenda kumzika Ruge

Kabla ya ibada ya mazishi jioni ya leo, mwili wa Ruge utaagwa kwenye viwanja vya Ghymkhana kijijini Kiziru