Baada ya kuagwa jijini Dar es salaam, mwili wa Ruge ulisafirishwa jana Jumapili kuelekea Bukoba tayari kwa mazishi hayo
Wananchi wengi walijitokeza uwanja wa Ndege wa Bukoba katika mapokezi ya mwili wa Ruge ambaye enzi za uhai wake alikuwa mtu wa watu
Watu wengi wamesafiri kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania kwenda kumzika Ruge
Kabla ya ibada ya mazishi jioni ya leo, mwili wa Ruge utaagwa kwenye viwanja vya Ghymkhana kijijini Kiziru