Wadau wapendekeza Harambee ya kuichangia Yanga

Ili kuongeza kasi ya uchangiaji wa klabu ya Yanga, baadhi ya wadau wamependekeza uongozi wa Yanga uandae ‘Harambee’ ambayo itakuwa ni siku maalumu kwa Wana Yanga kuichangia timu yao

Harambee hiyo inaweza kuandaliwa na kufanyika katika ukumbi utakaofaa ambapo utaratibu wa kutoa mwaliko kwa wadau wa Yanga unaweza kuandaliwa

Hapa waalikwe wananchi wa kawaida, watu maarufu, wafanyabishara, viongozi wa dini, viongozi wa Serikali kiufupi Yanga ina mtaji mkubwa wa watu, siku hiyo inaweza kutumika kuwaunganisha watu wote

Pia unaweza kuandaliwa utaratibu kwa tukio hilo kurushwa ‘mbashara’ katika runinga na redio mbalimbali ili wadau wengine ambao hawakualikwa waweze kushiriki kwenye Harambee hiyo kupitia vyombo vyao vya habari

Uchangiaji utafanyika ukumbini kwa kuwashirikisha wadau walioalikwa huku pia namba za kuchangia zikiendelea kutangazwa kwa wale wanaofuatilia kupitia vyombo vya habari ili waweze kuchangia

Utaratibu huu sio mgeni umekuwa ukitumiwa na watu binafsi na taasisi mbalimbali katika kuzishirikisha jamii zao linapokuja suala la uchangiaji wa fedha