YANGA vs ALLIANCE FC : Robo Fainali ASFC

Droo ya hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Azam (ASFC) imefanyika leo ambapo vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga watachuana na Alliance Fc katika mchezo wa robo fainali utakaopigwa kati ya March 25-28 2019
Mchezo huo utapigwa dimba la CCM Kirumba.

Hii itakuwa mara ya tatu kwa Yanga kuchuana na Alliance Fc msimu huu, mara ya pili kwa timu hizo kuchuana uwanja wa CCM Kirumba kwenye mwezi huu wa tatu

Kagera Sugar itakuwa nyumbani kuchuana na Azam Fc katika mchezo mwingine wa robo fainali wakati KMC itakuwa mwenyeji wa African Lyon.

Mchezo mwingine ni kati ya Lipuli Fc itakayokuwa nyumbani kupepetana na Singida United