Juuko ana kadi tatu za njano, Okwi mgonjwa, Nyoni hayuko ‘fit’

Katika orodha ya wachezaji 20 ambao jana walisafiri kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo dhidi ya JS Saoura yamekosekana majina ya wachezaji watatu muhimu ambao ni Juuko Murshidi, Erasto Nyoni na Emmanuel Okwi

Wakati Okwi aliondolewa kikosini kutokana na kuwa hajapona vizuri majeraha yake, Juuko anatumikia adhabu ya kadi za njano

Baada ya mchezo dhidi ya Stand United, kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alitaja sababu ya kutomtumia beki Erasto Nyoni ambaye ameanza mazoezi hivi karibuni akitoka kwenye majeraha ya goti

Aussems alisema Nyoni bado ‘hayuko fit’ na atahitaji muda zaidi ili kuweza kurejea kwenye kiwango chake.

Kutokana na umuhimu wa mchezo dhidi ya JS Saoura, Aussems amelazimika kusafiri na wachezaji ambao wana utimamu wa mwili kwa asilimia 100