Wakati Okwi aliondolewa kikosini kutokana na kuwa hajapona vizuri majeraha yake, Juuko anatumikia adhabu ya kadi za njano
Baada ya mchezo dhidi ya Stand United, kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alitaja sababu ya kutomtumia beki Erasto Nyoni ambaye ameanza mazoezi hivi karibuni akitoka kwenye majeraha ya goti
Aussems alisema Nyoni bado ‘hayuko fit’ na atahitaji muda zaidi ili kuweza kurejea kwenye kiwango chake.
Kutokana na umuhimu wa mchezo dhidi ya JS Saoura, Aussems amelazimika kusafiri na wachezaji ambao wana utimamu wa mwili kwa asilimia 100