NINJA : Afungiwa Mechi Tatu

Kamati ya Nidhamu ya TFF imemfungia mchezaji wa timu ya Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ kutocheza mechi tatu mfululizo baada ya kamati hiyo kubaini kuwa mchezaji huyo ametenda kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa timu ya Coastal Union katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara uliochezwa mkoani Tanga

Suala la Ninja liliamuliwa juzi katika kikao cha Kamati hiyo kilichoketi jijini Dar es salaam

Ninja atakosa mchezo wake wa kwanza dhidi ya Lipuli Fc, March 16 2019