Katika mahojiano na Radio UFM, Zahera amesema huwa anapanga kikosi chake kufuatana na mahitaji ya mpinzani anayekutana nae
“Kwa wanaofuatilia wanafahamu, sio Ajib tu ambaye huwa anapumzika, nimekuwa nikibadili wachezaji mara kwa mara kufuatana na mahitaji ya mchezo,” alisema Zahera
“Mabadiliko haya ni ya kawaida, haimaanishi kwamba Ajib kashuka kiwango au nina ugomvi nae”
“Wapo watu ambao kazi yao ni kufanya uchonganishi Yanga, nawashauri wafanye mambo mengine yenye faida kwao”
Baada ya kuwa na mwenendo mzuri tangu akabidhiwe kitambaa cha unahodha, Ajib amehusika kwa kucheza michezo mingi ya Yanga kabla ya michezo mitatu iliyopita ambayo yote hakuanza
Ajib amefunga mabao sita msimu huu na kutoa pasi za mabao 15.
Mpaka sasa ndiye mchezaji mwenye mafanikio zaidi kwenye ligi kwani kati ya mabao 45 ayliyofungwa na Yanga, Ajib amehusika katika mabao 21