
Wawa alipata majeraha ya kifundo cha mguu kwenye mchezo uliopita dhidi ya JS Saoura ambapo Daktari wa Simba Yassin Gembe alisema beki huyo raia wa Ivory Coast pamoja na kiungo Haruna Niyonzima walipata majeraha ya enka kutokana na mazingira ya uwanja wa Agosti 20 ambao una nyasi bandia
Wawa amesema hali yako imeimarika na atacheza mchezo wa Jumamosi
“Niko vizuri sasa, niliumia katika mechi iliyopita kule Algeria, lakini sasa ninaendelea vizuri na nitacheza mechi ya Jumamosi,” amesema
“Naamini tutafanya vizuri kwenye mchezo huo, tutapambana kwa sababu tunataka kuwafurahisha mashabiki wetu na vilevile tunataka kuweka rekodi ya kutinga robo fainali”
Wawa alishiriki mazoezi ya Simba yliyofanyika kwenye uwanja wa Boko Veterans jana jioni