
Aussems ambaye msimu huu ameiongoza Simba kwa mafanikio makubwa kwa kuweza kuipeleka hatua ya makundi, amedhamiria kuvuka malengo kwa kutinga robo fainali
“Mchezo huu muhimu kuchezwa katika uwanja wetu wa nyumbani mbele ya mashabiki wetu, inatuongezea kujiamini.
“Tuko katika nafasi nzuri zaidi ya kupata ushindi kuliko wapinzani wetu,” amesema Aussems
“Nafahamu mchezo hautakuwa mwepesi kwani wapinzani wetu nao wanahitaji ushindi ili wafuzu”
“Lakini sisi tuna faida ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa mashabiki wetu. Ni muhimu mashabiki wakajitokeza kwa wingi uwanjani, wajaze uwanja na watuunge mkono kwa muda wote wa mchezo, ushindi utakuwa upande wetu”
Mshindi wa mchezo kati ya Simba dhidi ya AS Vita atajihakikishia kutinga hatua ya robo fainali na timu itakayoshinda kwenye mchezo kati ya Al Ahly dhidi ya JS Saoura unaopigwa Misri
Matokeo ya sare yatazipa nafasi JS Saoura na Al Ahly kutinga robo fainali