
Nyoni aliyerejea kikamilifu baada ya kupona majeraha, amesema upande wao wachezaji wanajifua kikamilifu ili kuhakikisha wanashinda mchezo huo
“Mchezo huu ni fainali kwetu, tunahitaji kushinda ili tuweze kutinga robo fainali. Mawazo yetu yote yako katika mchezo huo,” amesema
“Tunahitaji sana sapoti ya mashabiki wetu. Tunajua wakija kwa wingi wataongeza hamasa kwetu na kutuongezea ari ya kupambana”
Kikosi cha Simba chini ya kocha Patrick Aussems na Msaidizi wake Denis Kitambi leo kimejifua kwenye uwanja wa Taifa ikiwa ni maandalizi yake ya mwisho kwenye uwanja huo kabla ya mchezo keshokutwa
Wapinzani wao AS Vital Club waliwasili jijini Dar es salaam jana ambapo leo wamefanya mazoezi katika viwanja vya Ghymkhana
Timu hiyo itajifua kwenye uwanja wa Taifa kesho