Mzee Akilimali augua Bagamoyo

Hali ya Mwanachama maarufu wa klabu ya Yanga Mzee Ibrahim Akilimali inaelezwa sio nzuri ambapo amelazwa Hospitali ya Baobab akiendelea na matibabu ya ugonjwa kisukari

Mzee Akilimali amewaomba wadau wa Yanga na Watanzania wote kwa ujumla wamuombee ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua

“Hali yangu sio nzuri. Niko huku Bagamoyo najiuguza maradhi ya kisukari. Mniombee kwani kisukari kinanitesa sana,” Mzee Akilimali amenukuliwa na Spoti Xtra

Mzee Akilimali ni miongoni mwa wanachama wa Yanga vinara wa kutoa maoni juu ya masuala mbalimbali ya klabu hiyo

Wakati mwingine hujikuta akiingia katika mgogoro na wanachama wenzake, wakimtuhumu kuwa ni mpinga maendeleo.