Aussems ataja sababu ya Juuko kuikosa AS Vita

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema beki wa Kimataifa wa Uganda Juuko Murshidi hatakuwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo kitakachoikabili AS Vita Club kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa utakaopigwa katika dimba la Taifa kesho.

Aussems amesema Juuko alipata majeraha na atahitaji kupumzika zaidi ili aweze kuwa sawa kabla ya kuanza kumtumia

“Juuko alipata majeraha, anahitaji kupumzika mpaka Jumatatu. Hivyo hakuna uwezekano wa kumtumia katika mchezo huo wa kesho,” amesema Aussems

Hata hivyo Aussems amethibitisha kuwa kiraka Erasto Nyoni yuko fit kuelekea mchezo huo

“Nyoni alianza mazoezi wiki iliyopita. Hatukusafiri nae kwenda Algeria ili kumpa muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa fit”

“Tumefanya nae mazoezi siku hizi mbili, bila shaka atakuwepo Jumamosi”

Nyoni na Okwi walijiunga katika mazoezi ya kikosi cha Simba juzi ambapo wanatarajiwa kujumuishwa katika kikosi kitakachoikabili AS Vita

Kiungo Jonas Mkude ataukosa mchezo huo akitumikia adhabu ya kadi mbili za njano