Kikosi cha Simba vs Ruvu Shooting Leo

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba mda mchache ujao watashuka katika dimba la Taifa kuikabili Ruvu Shooting kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amekifanyia mabadiliko kikosi kinachoshuka dimbani leo, akiwapa mapumziko baadhi ya wachezaji huku wengine wakikosekana kutokana na kukabiliwa na majukumu ya timu za Taifa

Habari njema ni kujumuishwa kwa kiungo Jonas Mkude na Meddie Kagere ambao watajiunga na majukumu ya timu za Taifa baada ya mchezo wa leo