
Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba ni miongoni mwa timu nane zinazosubiri kuwafahamu wapinzani wao katika hatua hiyo
Miongoni mwa kanuni zitakazotumika katika upangaji wa droo hiyo, timu zilizotoka kundi moja haziwezi kukutana katika hatua ya robo fainali
Kwa maana hiyo Simba haiwezi kukutana na Al Ahly kwenye hatua ya robo fainali
Pia timu zilizomaliza nafasi ya pili hatua ya makundi zitapangwa na timu zilizomaliza katika nafasi ya kwanza
Al Ahly, Wydad Casablanca, TP Mazembe na Esperance zimemaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao hivyo ukiondoa Al Ahly, Simba itapangiwa miongoni mwa timu tatu zitakazokuwa zimesalia