Simba kucheza na Wydad, TP Mazembe au Esperance robo fainali ligi ya mabingwa

Droo ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika inafanyika leo huko Misri, saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba ni miongoni mwa timu nane zinazosubiri kuwafahamu wapinzani wao katika hatua hiyo

Miongoni mwa kanuni zitakazotumika katika upangaji wa droo hiyo, timu zilizotoka kundi moja haziwezi kukutana katika hatua ya robo fainali

Kwa maana hiyo Simba haiwezi kukutana na Al Ahly kwenye hatua ya robo fainali

Pia timu zilizomaliza nafasi ya pili hatua ya makundi zitapangwa na timu zilizomaliza katika nafasi ya kwanza

Al Ahly, Wydad Casablanca, TP Mazembe na Esperance zimemaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao hivyo ukiondoa Al Ahly, Simba itapangiwa miongoni mwa timu tatu zitakazokuwa zimesalia