Simba vs TP Mazembe robo fainali ligi ya mabingwa

Droo ya hatua ya robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika imefanyika leo nchini Misri ambao mabingwa wa soka Tanzania Simba wamepangwa kucheza na TP Mazembe katika hatua hiyo ya robo fainali

Mchezo wa kwanza utapigwa jijini Dar es salaam April 05 huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, April 12 2019

Simba itasafiri kwenda nCongo kwa mara ya pili katika michuano ya mwaka huu mara ya kwanza ikicheza na AS Vita katika hatua ya makundi

Mamelodi Sundowns mabingwa wa mwaka 2016 wao wamepangwa kuchuana na Al Ahly, Horoya ikipangwa kuchuana na Wydad Casablanca wakati CS Constantine imepangwa kuchuana na Esperance

Katika droo hiyo Simba iliwakilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu Crescentius Magori na Mwenyekiti Swedi Mkwabi