
Mchezo wa kwanza utapigwa jijini Dar es salaam April 05 huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, April 12 2019
Simba itasafiri kwenda nCongo kwa mara ya pili katika michuano ya mwaka huu mara ya kwanza ikicheza na AS Vita katika hatua ya makundi
Mamelodi Sundowns mabingwa wa mwaka 2016 wao wamepangwa kuchuana na Al Ahly, Horoya ikipangwa kuchuana na Wydad Casablanca wakati CS Constantine imepangwa kuchuana na Esperance

Katika droo hiyo Simba iliwakilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu Crescentius Magori na Mwenyekiti Swedi Mkwabi