Wachezaji Simba wapewa mapumziko

Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting juzi, wachezaji wa kikosi cha Simba ambao hawakuitwa katika timu za Taifa walipewa mapumziko ya siku nne kabla ya kuendelea na maandalizi ya michezo inayofuata

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema baada ya kucheza mechi mfululizo kwa takribani mwezi mzima, wamewapa wachezaji mapumziko hayo ili waweze kuondoa uchovu

Simba inatarajiwa kuerejea mazoezini Jumatatu ijayo kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbao Fc ambao huenda ukapigwa dimba la Jamhuri mkoani Morogoro, March 31 2019

Uwanja wa Taifa unatarajiwa kufungwa baada ya mchezo kati ya Tanzania dhidi ya Uganda utakaopigwa Jumapili, March 24 2019