
Manara amesema ni zamu ya Stars kufuzu kwa fainali za AFCON 2019 baada ya kujaribu bila ya mafanikio kwa miaka 39.
Amewataka mashabiki wa soka nchini bila ya kujali timu zao, waungane kuipa nguvu Stars ili iweze kupata ushindi dhidi ya Uganda
Naye Mkuu wa Dar es salaam Mh Paul Makonda ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya uhamasishaji, amesema jukumu lake kubwa ambalo anaamini amelitekeleza ni kuiweka timu ya Taifa mikononi mwa Watanzania kuelekea mchezo dhidi ya Uganda
Akizungumza na Wanahabari kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere leo, Makonda amesema Watanzania wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa Jumapili
Amesema atahakikisha usafiri wa kutosha unakuwepo kutoka kila pembe ya jiji la Dar es salaam
“Daladala yoyote kutoka sehemu yoyote ya jiji la Dar es salaam, nawapa ruhusa ya kuendesha route ya kutoka popote walipo kwenda Uwanja wa Taifa. Ukipata shida yoyote njiani nitafute mimi,” amesema Makonda ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa jiji la Dar es salaam
“Tukishinda hii mechi nitakahikikisha tunafanya party kubwa sana ndani ya hili jiji la Dar na Tanzania kwa ujumla”
Mgeni rasmi wa mchezo huo atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa