
Samatta, kinara wa mabao ligi kuu ya Ubelgiji, amewatoa hofu Watanzania kuelekea mchezo huo akiahidi kuwa watafanya kile walichoelekezwa na Kocha Emmanuel Amunike ili waweze kuibuka na ushindi
“Tumefanya maandalizi ya kutosha. Tunafahamu mchezo hautakuwa mwepesi lakini tunayo kila sababu ya kutumia vyema uwanja wetu wa nyumbani kupata ushindi,” amesema Samatta
Matokeo ya ushindi dhidi ya Uganda yanaweza kuipa Stars nafasi ya kufuzu kwa fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika mwezi Juni nchini Misri.
Hata hivyo ili Stars iweze kufuzu lazima Cape Verde iifunge au itoke sare na Lesotho. Mchezo baina ya timu hizo utapigwa huko Cape Verde muda sawa na mchezo kati ya Stars dhidi ya Uganda utakaopigwa saa 12 jioni
Wapinzani wa Stars, Uganda Cranes wanatarajiwa kuwasili nchini leo
Uganda iliweka kambi ya wiki moja nchini Misri kujiandaa na mchezo huo