KAPOMBE: Kurejea Kikosini SIMBA SC

Beki wa pembeni wa Simba Shomari Kapombe ameruhusiwa kuanza mazoezi mepesi tayari kurejea dimbani baada ya kupona majeraha ya goti

Hivi karibuni Kapombe alikwenda Afrika Kusini kufanyiwa uchunguzi wa jeraha alilopata wakati akiitumikia timu ya Taifa mwishoni mwa mwaka jana

Habari njema ni kwamba madaktari wameridhishwa na uponaji wa jeraha hilo hivyo kumruhusu Kapombe kuanza mazoezi mepesi

Kiraka huyo aliyekuwa nje ya dimba kwa takribani miezi mitano, anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi wiki ijayo na huenda akarejea kikosini mapema kuwahi mchezo wa marudiano wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe utakaopigwa April 12 au 13 huko DR Congo