Zahera kuiwahi Alliance Fc

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera anatarajiwa kurejea Jumatano kuungana na kikosi cha timu hiyo kinachojiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Alliance Fc.

Jana Zahera akiwa kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, alikiongoza kikosi cha timu hiyo kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Liberia na kukata tiketi ya kufuzu fainali za AFCON 2019

Mwishoni mwa wiki hii Yanga itaelekea mkoani Mwanza kuikabili Alliance Fc katika mchezo utakaopigwa dimba la CCM Kirumba, March 30 2019

Kwa sasa Yanga inajifua chini ya kocha msaidizi Noel Mwandila