Kipenga kimepulizwa, fomu za uchaguzi Yanga zaanza kutolewa

Baada ya ‘figisu’ za uchaguzi kumalizika, hatimaye Wanayanga wana uhakika sasa kuwa mwezi ujao uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo utafanyika na viongozi wapya watapatikana katika nafasi zote

Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahela aliweka wazi kuwa uchaguzi utafanyika May 05 badala ya April 28 kutokana na siku hiyo kutakuwa na mchezo wa fainali za AFCON U17. Uchaguzi huo utasimamiwa na Yanga, wao TFF watakuwa waangalizi tu

Tayari kipenga kimepulizwa na leo fomu zinaanza kutolewa Makao Makuu ya klabu Mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam

Hii ni nafasi adhimu kwa Wanayanga kuijenga timu yao upya baada ya mateso ya takribani misimu miwili

Ni wakati kwa Wanachama wenye sifa na uwezo wa kuipeleka Yanga mbele kujitokeza kuchukua fomu

Aidha si vibaya kwa wanachama wengine kushawishiwa wachukue fomu kugombea pale tunapoona wanazo sifa na tuna imani nao

Huu ni wakati wa kuijenga Yanga imara ambayo itakuwa na mafanikio zaidi

Wanachama wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu na siku ya uchaguzi, haipaswi kufanya makosa kwa wapiga kura.

Wanachama watumie muda wao kuwasikiliza wagombea wote wakati wa kampeni ili waweze kuchagua viongozi ambao wataweza kuitoa Yanga hapa ilipo