Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahela aliweka wazi kuwa uchaguzi utafanyika May 05 badala ya April 28 kutokana na siku hiyo kutakuwa na mchezo wa fainali za AFCON U17. Uchaguzi huo utasimamiwa na Yanga, wao TFF watakuwa waangalizi tu
Tayari kipenga kimepulizwa na leo fomu zinaanza kutolewa Makao Makuu ya klabu Mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam
Hii ni nafasi adhimu kwa Wanayanga kuijenga timu yao upya baada ya mateso ya takribani misimu miwili
Ni wakati kwa Wanachama wenye sifa na uwezo wa kuipeleka Yanga mbele kujitokeza kuchukua fomu
Aidha si vibaya kwa wanachama wengine kushawishiwa wachukue fomu kugombea pale tunapoona wanazo sifa na tuna imani nao
Huu ni wakati wa kuijenga Yanga imara ambayo itakuwa na mafanikio zaidi
Wanachama wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu na siku ya uchaguzi, haipaswi kufanya makosa kwa wapiga kura.
Wanachama watumie muda wao kuwasikiliza wagombea wote wakati wa kampeni ili waweze kuchagua viongozi ambao wataweza kuitoa Yanga hapa ilipo