Gadiel arejea kutoka Afrika Kusini

Beki wa pembeni wa Yanga Gadiel Michael amerejea nchini mapema baada ya kumaliza majaribio yake katika klabu ya Bidvest Wits inayoshiriki ligi kuu nchini Afrika Kusini

Gadiel aliondoka wiki iliyopita kwenda Afrika Kusini baada ya kupata mwaliko kutoka Bidvest

Bado hakuna taarifa iliyotolewa kama amefuzu majaribio hayo au la