Yanga yarejea Dar kutoka Mtwara, kuunganisha Mwanza kesho

Kikosi cha Yanga kimewasili salama jijini Dar es salaam leo kikitokea mkoani Mtwara ambapo jana kililazimishwa sare ya bao 1-1 na Ndanda Fc

Vinara hao wa ligi kuu wanatarajia kukwea pipa kurejea mkoani Mwanza kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya African Lyon

Mchezo huo utapigwa April 08 katika uwanja wa CCM Kirumba