Dk Kigwangala mgeni rasmi mchezo wa Simba vs TP Mazembe

Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla atakuwa mgeni rasmi wa mchezo wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Simba dhidi ya TP Mazembe

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi, April 06 2019 katika uwanja wa Taifa saa kumi kamili jioni

Dk Kigwangala ambaye ni mdau mkubwa wa klabu ya Simba ataungana na maelfu ya mashabiki wa timu hiyo ambao kesho watafurika kuujaza uwanja wa Taifa ili kushuhudia mtanange huo