Gadiel, Ninja waongeza nguvu Yanga

Beki kisiki wa Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ amemaliza adhabu baada ya kukosa michezo mitatu hivyo yuko huru kuwatumikia vinara hao wa ligi kuu katika mchezo dhidi ya African Lyon

Kesho Jumatatu, Yanga itashuka katika dimba la CCM Kirumba kucheza mchezo wake wa kwanza wa nyumbani wakiwa nje ya jiji la Dar es salaam

Aidha beki wa upande wa kushoto Gadiel Michael Mbaga aliyekuwa Afrika Kusini kufanya majaribio kunako klabu ya Bidvest Wits, amerejea na huenda akawemo katika kikosi kitakachoikabili African Lyon kesho

Baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Ndanda Fc kwenye mchezo uliopita, Yanga itakuwa ikisaka matokeo muhimu ya ushindi ili kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi