SIMBA Yatuma malalamiko CAF – Mabadiliko ya Marefa

Klabu ya Simba kupitia kwa Mtendaji wake Mkuu Crescentius Magori, imeliandikia barua Shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) kufuatia mabadiliko ya waamuzi wa mchezo wa pili wa robo fainali ligi ya mabingwa kati ya TP Mazembe dhidi ya Simba

Mapema leo CAF ilitoa taarifa juu ya mabadiliko hayo ambayo yamefanyika siku tano kabla ya mchezo utakaopigwa April 13 Lubumbashi, DR Congo

TP Mazembe ndio iliyoomba kubadilishwa kwa waamuzi hao

Simba imeeleza hofu yake kwa mabadiliko hayo ya kushitukiza kuwa yasije yakawa na lengo baya

“Tumetuma malalamiko dhidi ya @CAF_Online kwa kufanya mabadiliko ya waamuzi wa mchezo wa marudiano wa #CAFCL ambao tutacheza Jumamosi. / We have formally lodged a complaint against CAF for the abrupt change in referees ahead of match against TP Mazembe in this Saturday in DRC”