Yanga yasaka alama tatu dhidi ya African Lyon leo

Vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga leo watakuwa uwanja wa CCM Kirumba kuikabili African Lyon

Huo utakuwa mchezo wa kwanza wa nyumbani kwa Yanga kuchezwa nje ya jiji la Dar es Salaam msimu huu

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema baada ya kulazimishwa sare mchezo uliopita dhidi ya Ndanda Fc, leo wanahitaji alama zote tatu

Viingilio vya mchezo huo ni Tsh 3,000/- kwa majukwaa ya kawaida na Tsh 10,000/- upande wa VIP