Yanga hakuna kulala, yajifua kuikabili Kagera Sugar

Licha ya kushuka dimbani jana, vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Yanga wanakabiliwa na mchezo mwingine dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa keshokutwa Alhamisi April 11 2019 kwenye uwanja wa CCM Kirumba

Kikosi cha Yanga leo kimeendelea na mazoezi katika uwanja wa CCM Kirumba kujiandaa na mchezo huo

Kocha Mwinyi Zahera amesema watahakikisha wanashinda michezo yote nane iliyobaki ili kujiwekea mazingira ya kutwaa ubingwa kwani anaamini upo uwezekano mkubwa kwa Simba kupoteza baadhi ya michezo kutokana na ugumu wa ratiba itakayowakabili kama TFF haitawapendelea