Kagera Sugar ilitangulia kufunga bao la kuongoza kwenye dakika ya 30 likiwekwa kambani na Paul Ngalyoma aliyeunganisha kwa kichwa mpira wa kona
Dakika nne baadae Yanga ilisawazisha bao hilo baada ya Kassim Khamis kujifunga wakati akijaribu kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Papi Tshishimbi
Mpaka wakati wa mapumziko matokeo yalikuwa 1-1

Yanga ilihitaji dakika tatu tu za kipindi cha pili kuandika bao la pili lililowekwa kimiani na Heritier Makambo aliyeunganisha kwa kichwa mpira wa juu uliovushwa na Kelvin Yondani
Kagera Sugar wakasawazisha tena kwenye dakika ya 58 baada ya shuti la Kassim Khamis kumshinda mlinda lango Klaus Kindoki na kutinga kimiani
Kiungo Thabani Kamusoko aliihakikishia Yanga alama tatu muhimu baada ya kufunga bao la tatu kwenye dakika ya 72
Kamusoko aliukwamisha nyavuni mpira wa adhabu kwa ustadi mkubwa
Kwenye dakika ya 82 Yanga ilipata pigo baada ya kelvin Yondani kuonyeshwa kadi nyekundu kufuatia tukio la kumpiga kiwiko mchezaji wa Kagera Sugar
Matokeo hayo yameifanya Yanga ifikishe alama 74 na kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama 11 dhidi ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili