Makambo amuwashia taa nyekundu Aiyee

Bao alilofunga Heritier Makambo leo limemfanya mshambuliaji huyo Mcongoman afikishe mabao 15 akimuacha Meddie Kagere wa Simba mwenye mabao 14.

Leo Makambo aliisaidia Yanga kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 3-2 dhidi ya Kagera Sugar

Makambo sasa anahitaji kufunga bao moja zaidi ili aweze kumfikia Salim Aiyee wa Mwadui Fc anayeongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 16

Katika michezo miwili iliyopita, Makambo ameifungia Yanga mabao matatu